Utoto unaelezwa ni ule wa rika kati ya siku moja hadi miaka 15,baada ya hapo mtoto hubadilika jina na kuitwa kijana, ujana ni kuanzia kati ya miaka 18- 45, hili ndilo hasa rika kamili la ujana kadri nijuvyo.
Kwa mujibu wa Shaaban Robert kijana ni Taifa la leo.
Taifa la leo kwa mantiki ya kuwa nguvu kazi na tegemezi kuu katika wakati uliopo ili ajenge nchi na kutumika ipasavyo katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Ukweli unaoonyesha kuwa vijana katika Afrika na hasa Visiwani Zanzibar ni mithili ya tingatinga au greda linaloweza kufumua vifusi, miamba, milima na hatimaye kunyoosha njia iliyokuwa na tabu ya mashimo, mabonde na makorongo makubwa kisha waruhusiwe wazee kupita na kujinafasi buheri hamsa wa ishirini.
Katika nchi nyingi za kiafrika Vijana hutumiwa kama mihuri ya kuhalalishia tawala za wazee.
Jambo hilo pengine ndilo linalowafanya wazee hao baada ya kuzeeka laana ya kulichukia rika la ujana huwangukia na kuanza kupigwa vigongo vya utosi. Hapana nieleweke sihimizi mauaji ya vikongwe.
Nimejikuta nikilazimika kuyaandika makala haya huku nikiawa na kumbukumbu nyingi ndani ya kichwani changu kabla na baada ya Mapinduzi ya 1964 Visiwani Zanzibar.Kila nikilitazama kundi au rika la Vijana lilivyotumikishwa na linavyotumikishwa, nashindwa kuwatofautisha wao na matumizi ya kondomu kwa binadamu.
Katika nchi nyingi za kiafrika Vijana hutumiwa kama mihuri ya kuhalalishia tawala za wazee.
Jambo hilo pengine ndilo linalowafanya wazee hao baada ya kuzeeka laana ya kulichukia rika la ujana huwangukia na kuanza kupigwa vigongo vya utosi. Hapana nieleweke sihimizi mauaji ya vikongwe.
Nimejikuta nikilazimika kuyaandika makala haya huku nikiawa na kumbukumbu nyingi ndani ya kichwani changu kabla na baada ya Mapinduzi ya 1964 Visiwani Zanzibar.Kila nikilitazama kundi au rika la Vijana lilivyotumikishwa na linavyotumikishwa, nashindwa kuwatofautisha wao na matumizi ya kondomu kwa binadamu.
Ni mja gani huyo mjinga anayeweza kuithamini kondom ikiwa hana haja nayo kwa wakati maalumu mahali fulani na kwasababu husika? Hata kuibeba huwa ni aibu na fedheha isiyomithilika.
Katika historia ya kweli vijana ndiyo walioamsha vuguvugu la kutaka mabadiliko ya haraka baada ya kuchoshwa na ukandamiziaji uliokuwa ukifanywa na wageni waliokuwa wakiwabagua waafrika walio wengi na kuwanyima baadhi ya fursa muhimu.
Umoja wa vijana wa chama cha ASP, ASP Youth League hapa Zanzibar ulikuwa mstari wa mbele kushajihisha hamasa za kisiasa baina ya mashamba na maeneo ya mijini huko Pemba na Unguja na kuweka mikakati ya kuudondosha utawala wa kisultan madarakani.
Siku ya Mapinduzi, vijana ndio waliokuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nchi inabaki mikononi mwa wazalendo, lakini cha kushangaza kundi la wazee likajitokeza na kujihesabu kuwa wao ndiyo waliokuwa mstari wa mbele katika Mapinduzi.
Hata Mzee Abeid Karume alikiri kwamba hakuwamo katika kundi la watu wanaoitwa ‘Member of 14’ wakati Mapinduzi yakifanyika na kwamba siku alikuwa amejificha Dar es Salaam kwa sababu za kiusalama.
Ni jambo la kweli wazee wa ASP kwamba walishiriki kupanga na kufanya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 lakini ikumbukwe pia na iaminike kuwa walioshiriki kikamilifu katika mapambano ya ana kwa ana na ya kufa na kupona ni kundi kubwa la vijana.
Baada ya Mapinduzi kufanikiwa wazee karibu wote ndiyo walioshika madaraka ya juu katika SMZ ikiwamo wao kuwa MBM, mawaziri, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu na makamishna. Vijana wakajikuta wakitiwa mchanga wa macho.
Hata hivyo, sehemu kubwa ya wanasiasa vijana waliokuwa hodari na wasomi walipotea katika mazingira ya utatanishi ulioambatana na chuki na hadi leo hii hawajulikani kama wako hai,wamezeeka sana au wako katika gereza fulani hapa Zanzibar au huko Tanganyika.
Katika historia ya kweli vijana ndiyo walioamsha vuguvugu la kutaka mabadiliko ya haraka baada ya kuchoshwa na ukandamiziaji uliokuwa ukifanywa na wageni waliokuwa wakiwabagua waafrika walio wengi na kuwanyima baadhi ya fursa muhimu.
Umoja wa vijana wa chama cha ASP, ASP Youth League hapa Zanzibar ulikuwa mstari wa mbele kushajihisha hamasa za kisiasa baina ya mashamba na maeneo ya mijini huko Pemba na Unguja na kuweka mikakati ya kuudondosha utawala wa kisultan madarakani.
Siku ya Mapinduzi, vijana ndio waliokuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nchi inabaki mikononi mwa wazalendo, lakini cha kushangaza kundi la wazee likajitokeza na kujihesabu kuwa wao ndiyo waliokuwa mstari wa mbele katika Mapinduzi.
Hata Mzee Abeid Karume alikiri kwamba hakuwamo katika kundi la watu wanaoitwa ‘Member of 14’ wakati Mapinduzi yakifanyika na kwamba siku alikuwa amejificha Dar es Salaam kwa sababu za kiusalama.
Ni jambo la kweli wazee wa ASP kwamba walishiriki kupanga na kufanya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 lakini ikumbukwe pia na iaminike kuwa walioshiriki kikamilifu katika mapambano ya ana kwa ana na ya kufa na kupona ni kundi kubwa la vijana.
Baada ya Mapinduzi kufanikiwa wazee karibu wote ndiyo walioshika madaraka ya juu katika SMZ ikiwamo wao kuwa MBM, mawaziri, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu na makamishna. Vijana wakajikuta wakitiwa mchanga wa macho.
Hata hivyo, sehemu kubwa ya wanasiasa vijana waliokuwa hodari na wasomi walipotea katika mazingira ya utatanishi ulioambatana na chuki na hadi leo hii hawajulikani kama wako hai,wamezeeka sana au wako katika gereza fulani hapa Zanzibar au huko Tanganyika.
Inaaminika kuwa kupotea na kuyayuka kwao kulitokana na hofu iliyowajaa wazee ili wasiwekwe pembeni katika kuiendesha nchi kutokana na wao kuwa na elimu kidogo na wengine kukosa miwani kabisa.
Kundi la vijana kwa mara ya kwanza lilipewa nafasi na Rais wa Awamu ya Pili, Zanzibar Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi alipoamua bila ya hofu kuwapa vyeo na kuwaingiza serikalini baadhi ya vijana hodari wakiwamo Seif Sharif Hamad, Salmin Amour Juma, Khatib Hassan Khatib, Soud Yussuf Mgeni na Omar Ramadhan Mapuri.
Kundi hili la mrengo wa kushoto kwa sehemu kubwa lilithbutu kunyoosha vidole vyao juu na kuhitaji yafanyike mabadiliko zaidi wakati huo likijiita ‘Progressive Team’ huku likichuana kwa nguvu ya hoja na lile la wazee lililokuwa likiitwa Liberators Mob.
Kundi la vijana kwa mara ya kwanza lilipewa nafasi na Rais wa Awamu ya Pili, Zanzibar Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi alipoamua bila ya hofu kuwapa vyeo na kuwaingiza serikalini baadhi ya vijana hodari wakiwamo Seif Sharif Hamad, Salmin Amour Juma, Khatib Hassan Khatib, Soud Yussuf Mgeni na Omar Ramadhan Mapuri.
Kundi hili la mrengo wa kushoto kwa sehemu kubwa lilithbutu kunyoosha vidole vyao juu na kuhitaji yafanyike mabadiliko zaidi wakati huo likijiita ‘Progressive Team’ huku likichuana kwa nguvu ya hoja na lile la wazee lililokuwa likiitwa Liberators Mob.
Wazee walikuwa ni kina Abdallah Natepe, Hassan Nassor Moyo, Jamal Ramadhan Nassib, Ramadhan Haji Faki, Khamis Daruwesh na wengine.
Kundi la vijana lililokuja kuwa imara kabla ya kugawanywa kwa fitna na vitisho lilikuwa la kina Ali Ameir Mohamed, Shaaban Khamis Mloo, Ali Haji Pandu, Isaac Sepetu, Adam Mwakanjuki, Salmin Amour na wengine.
Wazee kwa kiasi kikubwa na mara zote waliwatuhumu na kuwabatiza Vijana hao majina mabaya na kudai kwamba ni kundi la wasaliti na mamluki wapya wanaotaka kuyatosa na kuyapoteza Mapinduzi ili kuurejesha usultan visiwani Zanzibar.
Awamu ya tatu ilipofika, kidogo chini ya Rais Ali Hasssan Mwinyi kwa kipindi kifupi ilikuja na mkakati wa kuzibeba sura mpya katika kundi la vijana hao na kufanikiwa lakini awamu ya tano, sita na saba hofu ya vijana ikawapata tena watawala wetu.
Dk. Shein ameanza kulitosa kundi la vijana, lakini na yeye asishangae wala kustaajabu ikiwa nao wataamua na kujipanga ili kumpotezea mwaka 2015.
Kundi la vijana lililokuja kuwa imara kabla ya kugawanywa kwa fitna na vitisho lilikuwa la kina Ali Ameir Mohamed, Shaaban Khamis Mloo, Ali Haji Pandu, Isaac Sepetu, Adam Mwakanjuki, Salmin Amour na wengine.
Wazee kwa kiasi kikubwa na mara zote waliwatuhumu na kuwabatiza Vijana hao majina mabaya na kudai kwamba ni kundi la wasaliti na mamluki wapya wanaotaka kuyatosa na kuyapoteza Mapinduzi ili kuurejesha usultan visiwani Zanzibar.
Awamu ya tatu ilipofika, kidogo chini ya Rais Ali Hasssan Mwinyi kwa kipindi kifupi ilikuja na mkakati wa kuzibeba sura mpya katika kundi la vijana hao na kufanikiwa lakini awamu ya tano, sita na saba hofu ya vijana ikawapata tena watawala wetu.
Dk. Shein ameanza kulitosa kundi la vijana, lakini na yeye asishangae wala kustaajabu ikiwa nao wataamua na kujipanga ili kumpotezea mwaka 2015.
Sijajua ni kwa sababu gani hasa inayowasibu na kuwajaza woga usiokadirika viongozi wazee kuwatenga vijana, pengine ninachoweza kusema ni kuhofia ujio wa mabadiliko kwa mwendo wa haraka na kuwashangaza wazee hao ambao baadhi yao sasa wanajikongoja wakipungukiwa nguvu, maarifa na kusimamia maamuzi magumu.
Matumaini makubwa ya vijana yalikuwa ni kwa Rais mpya Dk. Ali Mohamed Shein.
Matumaini na matarajio hayo sasa yamezamishwa katika mkondo mkali wa Nungwi na hayaonekani kuwapa nafuu tena kwa upande wa vijana.
Uteuzi wake ulioanzia katika nafasi za kisiasa na kitaaluma bada ya kuukwa urais anaonekana kuwababeba wazee wenziwe na kuwatosa vijana ambao aliwatumia bila kuchoka katika hamsa za kumfanyia kampeni hadi kupata ushindi uliomweka Ikulu.
Matumaini makubwa ya vijana yalikuwa ni kwa Rais mpya Dk. Ali Mohamed Shein.
Matumaini na matarajio hayo sasa yamezamishwa katika mkondo mkali wa Nungwi na hayaonekani kuwapa nafuu tena kwa upande wa vijana.
Uteuzi wake ulioanzia katika nafasi za kisiasa na kitaaluma bada ya kuukwa urais anaonekana kuwababeba wazee wenziwe na kuwatosa vijana ambao aliwatumia bila kuchoka katika hamsa za kumfanyia kampeni hadi kupata ushindi uliomweka Ikulu.
Vijana wa leo si wale wa baada ya Mapinduzi ya Zanzibar 1964, ni wasomi, wepesi, wachapakazi na wajuzi katika fani mbalimbali, Rais Dk. Shein amefuumba macho yake na kuteua wastaafu kama kwamba hakuna vijana wapywa na wataalamu
Nimneona nimtumie salamu za haraka Dk. Shein na kumtaka atanabahai ili kufuata nyayo za Rais Jakaya Kikwete wa Tanganyika ambaye amekubali kuteua na kuwapa nafasi nyeti katika Serikali yake sehemu kubwa ya kundi la vijana.
Katika Ofisi za Serikali huko Tanganyika leo hii kuanzia kwenye halmashauri za wilaya, manispaa, ofisi za wakuu wa wilaya na mikoa na kwenye wizara za Serikali Kuu kumetamalaki vijana wasomi ingawaje na baadhi ya wazee wapo wakiwashindikiza vijana wao.
Ni kinyume kabisa cha mambo yalivyo hapa Zanzibar. Vijana wametiwa chachu na huachwa wapige maneno mabarazani, wamezoea kulambishwa pipi huku baadhi yao wakijilia urojo na wengine wakiamua kubwia unga na kujiajiri katika ajira hatarishi.
Nimneona nimtumie salamu za haraka Dk. Shein na kumtaka atanabahai ili kufuata nyayo za Rais Jakaya Kikwete wa Tanganyika ambaye amekubali kuteua na kuwapa nafasi nyeti katika Serikali yake sehemu kubwa ya kundi la vijana.
Katika Ofisi za Serikali huko Tanganyika leo hii kuanzia kwenye halmashauri za wilaya, manispaa, ofisi za wakuu wa wilaya na mikoa na kwenye wizara za Serikali Kuu kumetamalaki vijana wasomi ingawaje na baadhi ya wazee wapo wakiwashindikiza vijana wao.
Ni kinyume kabisa cha mambo yalivyo hapa Zanzibar. Vijana wametiwa chachu na huachwa wapige maneno mabarazani, wamezoea kulambishwa pipi huku baadhi yao wakijilia urojo na wengine wakiamua kubwia unga na kujiajiri katika ajira hatarishi.
Dk. Shein akumbuke na ajaribu kuvuta picha ya wakati wa kampeni zake akiwa Pemba na Unguja, ni kina nani hasa waliokuwa wakijaza kwenye magari na kupeperusha bendera ya chama kilichompa ushindi, ni wazee au vijana?
Kitendo chake cha kuendelea kuzifanya ajira za Serikali kama zenye hatimiliki kwa kundi moja la watu wenye itikadi ile ile anayoitii yeye ni kwenda kinyume cha ukweli wa mambo ulivyo,hii ni hatari nyeusi katika siku zijazo.
Vijana ni vijana wako wengi na wanahitaji kuangaliwa na kusikilizwa. Wakifumbwa midomo iko siku wataifumbua na hawataiziba ng’o.
Vijana wa Zanzibar ni wavumilivu sana, wastaarabu, wenye heshima, wengi kati yao wameamua kusafiri na kuishi ughaibuni, hawakutaka kuitegemea Serikali yao hivyo ni vema kwa hawa wachache waliopo wakasaidiwa na kupewa vijikazi.
Kitendo chake cha kuendelea kuzifanya ajira za Serikali kama zenye hatimiliki kwa kundi moja la watu wenye itikadi ile ile anayoitii yeye ni kwenda kinyume cha ukweli wa mambo ulivyo,hii ni hatari nyeusi katika siku zijazo.
Vijana ni vijana wako wengi na wanahitaji kuangaliwa na kusikilizwa. Wakifumbwa midomo iko siku wataifumbua na hawataiziba ng’o.
Vijana wa Zanzibar ni wavumilivu sana, wastaarabu, wenye heshima, wengi kati yao wameamua kusafiri na kuishi ughaibuni, hawakutaka kuitegemea Serikali yao hivyo ni vema kwa hawa wachache waliopo wakasaidiwa na kupewa vijikazi.
Wakiendelea kubaki vijiweni na mabarazani toka asubuhi hadi jioni wanaweza kupotoka, wanaweza kuamua kufanya uasharati,umalaya na kucheza kiduku huku wazee wao wakitanua kwa kukaangiza pilau ya michele ya basmati huku vijana wakila wali uliopikwa kwa mchele wa mapembe na kitoweo cha dagaa la kuosha.
Nafasi pekee ambayo nilifikiri Rais Dk. Shein ingeliweza kumpatia umaarufu na kujijengea matumaini ya matumaini ya kuungwa mkono zaidi ni kuligusa kundi hili, kulipa imani kundi la vijana na kuwaajiri katika nafasi za juu serikalini.
Angefanya hayo, angehesabiwa amelamba turufu na kujenga mtaji usio na shaka ifikapo mwaka 2015 kama angeamua sasa kuteua vijana wapya na kuwapa nafasi serikalini.
Ninamheshimu sana Dk. Shein, ni mtu makini, anyefuata taratibu, si mtu anayetegemea siasa za udaku na umbea. Anathamini Umoja wa Kitaifa lakini kwa kuliweka pembeni kundi la vijana naona kama anatamani asitoke mrisi katika mchezo wa karata katika uchaguzi ujao.
Nafasi pekee ambayo nilifikiri Rais Dk. Shein ingeliweza kumpatia umaarufu na kujijengea matumaini ya matumaini ya kuungwa mkono zaidi ni kuligusa kundi hili, kulipa imani kundi la vijana na kuwaajiri katika nafasi za juu serikalini.
Angefanya hayo, angehesabiwa amelamba turufu na kujenga mtaji usio na shaka ifikapo mwaka 2015 kama angeamua sasa kuteua vijana wapya na kuwapa nafasi serikalini.
Ninamheshimu sana Dk. Shein, ni mtu makini, anyefuata taratibu, si mtu anayetegemea siasa za udaku na umbea. Anathamini Umoja wa Kitaifa lakini kwa kuliweka pembeni kundi la vijana naona kama anatamani asitoke mrisi katika mchezo wa karata katika uchaguzi ujao.
No comments:
Post a Comment