Friday, 6 May 2011

Mji wa Homs walengwa na vifaru

Watu wasiopungua 1000 waliimba nyimbo za kuunga mkono wenzao wa mji wa Deraa ulio kusini mwa nchi ambako vikosi vimekuwa vikiwakamata mamiya ya wanaume katika misako ya nyumba hadi nyumba.
 Rais Assad achukiwa
picha yachomwa
Kote nchini Syria watu 2,843 inaaminika wamekamtwa na kufungwa. Wanaharakati wanasema kuwa idadi kamili huenda ni watu 8000 ambao wamekabiliwa na mateso kutoka majeshi.
''Marekani yasema hatua ya Syria ni unyama''
Makundi ya kutetea haki yamesema kuwa takriban watu 560 wameuawa kote nchini katika maandamano dhidi ya utawala dhalimu wa Rais Bashar al-Assad.
Maandamano yaliyoanza tarehe 15 mwezi Machi, ndiyo tishio kubwa kuwahi kutokea katika miaka arobaini ya utawala wa familia ya Assad katika mojapo ya nchi zenye sera ya kuwabana wananchi kwa sheria kali kupindukia.

No comments: