Manchester United itakutana na Barcelona kwenye fainali ya klabu Bingwa Ulaya baada ya kuichapa Schalke 04 ya Ujerumani kwa magoli 4-1.
Man United
Magoli ya Manchester United yalifungwa na Antonio Valencia, Darron Gibson, na Anderson kufunga magoli mawili.
Katika mchezo wa kwanza Man United ilipata ushindi wa mabao 2-0.
Barcelona iliingia fainali baada ya kuifunga Real Madrid 3-1 baada ya michezo miwili ya nusu fainali.
Fainali ya Klabu Bingwa Ulaya itachezwa kwenye uwanja wa Wembley, tarehe 28 mwezi Mei.
No comments:
Post a Comment